Waters of LifeBiblical Studies in Multiple Languages |
|
Home Bible Treasures Afrikaans |
This page in: -- Afrikaans -- Arabic -- Armenian -- Azeri -- Bengali -- Bulgarian -- Cebuano -- Chinese -- English -- French -- Georgian -- Greek -- Hausa -- Hebrew -- Hindi -- Igbo -- Indonesian -- Javanese -- KISWAHILI -- Malayalam -- Polish -- Portuguese -- Russian -- Serbian -- Somali -- Spanish -- Tamil -- Telugu -- Turkish -- Urdu? -- Yiddish -- Yoruba
Previous Lesson -- Next Lesson WARUMI - BWANA NDIYE HAKI au UADILIFU WETU
Masomo kuhusu Barua ya Paulo kwa Warumi
SEHEMU 1 - HAKI YA MUNGU INAHUKUMU WENYE DHAMBI WOTE NA KUJALIA HAKI PAMOJA NA KUWATAKASA WOTE WAMWAMINIO KRISTO (Warumi 1:18 - 8:39)
D - Uwezo Wa Mungu Hutuokoa Na Nguvu Ya Dhambi (Warumi 6:1 - 8:27)
2. Uhuru kutoka kwa sheria inarahisisha ukombozi wetu na dhambi (Warumi 6:15-23)WARUMI 6:15-22 Maswali ya ujanja ya Wayahudi aliyasikia yakilia tena ndani ya kumbukumbu ya Paulo: Je, tutende dhambi, kwa sababu hatuwi chini ya sheria, bali tumeokolewa kwa neema ? Paulo alikataa kata kata swali hilo la kishetani, maana lilitengenezwa si kwa Roho Mtakatifu, lakini kwa ajili ya mambo fulani tu. Paulo aliwashuhudia waumini kwamba, kwa mapenzi yao wenyewe walijitoa kabisa kwa kumtumikia Kristo kwa sababu ya upendo wake, na kwa sababu hiyo walipata kuwekwa huru na nguvu ya dhambi na madai ya sheria, wakibeba maisha ya haki ya Mungu ndani yao. Yeyote anayedai habari ya uhuru wa kibinadamu bila kumstahi Mungu atakuwa ni mwongo. Daktari Luther alikuwa akifananisha mtu na punda, alipotoa tamko kwamba, mtu mmoja peke yake hawezi kuishi bila bwana mkubwa, kwa sababu anahitaji fulani ampande na kuchukuliwa naye. - Wewe basi, umepandwa na mmojawapo, ni shetani au Mungu. Mungu anapopata kuwa Mungu wako, nawe unambeba kwa furaha, pia na kumtumikia kwa furaha na uangalifu, ndipa hali ya kukata tamaa, dhambi na nguvu ya mauti yanakoma ndani yako, Badala yake tumaini, amani na uhuru wa kweli ya rohoni yanaanza ndani yako. Kristo atakuwa amekuweka huru - si kwa ajili ya kupata wasiwasi au kujifurahisha tu, lakini kwa ajili ya kumtumikia Mungu, pia na kwa kutenda mema kwa wengine chini ya uongozi wa roho ya hali ya kujaliwa haki. Kwa njia ya utii kwa uongozi wa Roho Mtakatifu dhamiri yako itakuwa inatulia. Bila ushirikiano huo ndani ya Roho wa Kristo utadumu katika hali ya kukata tamaa na taabu. Kristo mwenyewe alishuhudia kwamba, alibeba nira, iwapo yeye mwenyewe alikuwa huru na kuwa Mungu wa milele. Hata hivyo, kwa furaha alijitwisha nira ya Babaye, na akamtii hadi kufa, tena kifo cha msalabani. Upendo tukufu ulimfanya Yesu kuwa mtumwa wa kupeleka mbali dhambi za ulimwengu. Basi, kwa nini wewe hujakubali kumfuata yeye? Je, wewe unabeba dhambi za marafiki zako na kuteseka kwa sababu ya ulegevu wao? Basi, usikasirike kwa ajili ya swali hilo; lakini weka moyo wako kwenye shabaha ya wokovu wao na wapate kuwekwa huru kiroho. Upendo wa Mungu unakusukuma kwenye ukombozi wa watu wote. Maisha pamoja na Kristo yanakuongoza kuwahudumia wengi, si kimawazo tu au kwa mhemuko kimoyo, lakini kwa mpango kamili, kwa kujitoa kabisa na kwa nguvu zako zote. Jinsi ulivyotumia zamani muda, fedha na vipawa vyako kwenye mambo ya kujifurahisha tu yasiyofaa, sasa basi tumia uwezo wako wote katika kumtumikia Kristo na wokovu wa watu wengine. Uwafariji wale wanaohuzunika, watembelee wagonjwa, wasaidie walio na njaa, jifunza na wale walio wadhaifu kimasomo, na uwape nuru wale wanaotafuta kujaliwa haki kwa njia ya injili. Upendo wa Kristo unaoonekana maishani mwa waumini ndiyo tumaini lenye subira ndani ya dunia yetu isiyo na haki. Je, umepata kuwa mtumishi wa Mungu na mtumwa wa upendo wa Mwana wake? Kama ndiyo, basi dhambi haiwezi kuwa na nguvu tena juu yako, kwa vile umepita ndani ya kifo cha ungamo, hali umesulibiwa na Kristo, ndipo umejazwa na Roho Mtakatifu wa kwake na kuimarishwa ndani ya uzima wake wa milele. Basi, unayo tumaini kuu pamoja na wote hao wanaoishi ndani ya Kristo. WARUMI 6:23 Mstari huu ni kama dhahabu, inajumlisha injili yote kamili, ukitueleza wazi matunda ya mwanadamu wa asili, na upande wa pili hilo jambo kuu linalopatikana kwake Kristo.
SALA: Tunakuabudu, Ee Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, kwa sababu umetuondoa kutoka katika uhusiano na dhambi na chuki, ulituweka huru na mapingu ya mauti, ulitubeba hadi kwenye mapana ya baraka ya Kristo, nawe ulitujaza na uhai wa Roho yako Mtakatifu, ili tusife kwa milele, bali tuishi nawe na ndani yako kutokana na neema yako kuu. Amina. SWALI:
|